• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wananchi wahimizwa kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa,wasiende kwenye ramli

Posted on: July 16th, 2019

Wananchi wamehimizwa kujiunga kwa wingi na mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa ili wapate vitambulisho vitakavyowasaidia kupata matibabu kwa mwaka mzima katika vituo vya kutolea huduma za Afya ikiwemo na Hospitali za Rufaa.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizindua Kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa mapema leo tarehe 16/07/2019, katika kijiji cha Ilobashi, kata ya Masengwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, amesema Bima ya Afya inawasaidia wananchi kuwa na uhakika wa matibabu kwa bei nafuu kwa mwaka mzima.

Amesema, wananchi wakiwa na uhakika wa matibabu, maradhi yakiwakuta hawana fedha hawatakuwa na mawazo ya kwenda kupiga ramli chonganishi kwa sababu tayari wana vitambulisho " Tusirudi huko ndugu zangu, kwenye kupiga ramli" amesisitiza Mhe. Telack.

Mhe. Telack amewaasa pia wananchi ambao vitambulisho vyao vimekwisha muda wake walipie tena kwa mwaka huu ili waendelee kupata matibabu huku akiwakumbusha Waganga wafawidhi wa vituo vyote vya Afya kuhakikisha dawa na vifaa vinakuwepo .

"Serikali inataka Watanzania wote wanakuwa na Bima za Afya ili kuweza kutibiwa kwa wakati, ubora na kwa bei nafuu, hakikisheni madirisha ya wagonjwa wa CHF yanakuwepo na yanafanya kazi kama ilivyo kwa madirisha ya wazee" amesema Telack.

Naye Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga aliyembatana na Mkuu wa Mkoa katika uzinduzi huo, amewasisitiza wakulima wote kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya mara tu watakapouza pamba ili wawe na uhakika wa matibabu.

"Kazi ya kilimo ina mchango mkubwa kwa pato la Taifa, asilimia 28.7 inatokana na kilimo,  hivyo siku hii ni muhimu sana kwa wakulima na mimi nasema, huwezi kulima kama huna Afya nzuri" amesema Mhe. Hasunga.

Wakiwahamasisha wananchi wengine kujiunga na mfuko huu, Bw. William Gwisu na Salu Izengo ambao wameshajiunga kwa muda mrefu, wameeleza mafanikio makubwa waliyoyapata kutokana na kujiunga ikiwemo kuokoa fedha nyingi baada ya kulazimika kupewa rufaa kwenye Hospitali kubwa.

Mkoa wa Shinyanga ni moja ya Mikoa mitatu nchini ambapo mradi wa CHF iliyoboreshwa umetekelezwa, Mikoa mingine ni Dodoma na Morogoro. Jumla ya Wananchi  

25,513 kati ya 261,608 wameshajiunga na mfuko huu tangu ulipozinduliwa rasmi Mkoani hapa tarehe 4 Oktoba, 2018.

                                                                                       Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya katika Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Rashid Mfaume 

                                                                                       akitoa taarifa ya CHF kabla ya uzinduzi wa Kampeni ya uhamasishaji wananchi kujiunga 

                                                                                       na mfuko huo leo katika kijiji cha Ilobashi, kata ya Masengwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

                                                                                          Meneja Mradi wa CHF uliokuwa unafadhili shughuli za uhamasishaji katika Mkoa wa Shinyanga, 

                                                                                          chini ya shirika la HPSS, Dkt. Harun Masare akitoa taarifa ya mradi na kuwaaga rasmi 

                                                                                          wananchi baada ya kukamilisha kazi hiyo kwa miaka mitano Mkoani hapa ambapo 

                                                                                          awamu ya kwanza inakamilika mwezi Julai mwaka huu

                                                                                    Wanafunzi wa Shule ya msingi Ilobashi wakitoa burudani ya nyimbo za kuhamasisha 

                                                                                    kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa CHF mbele ya mgeni rasmi (hayupo Pichani)

                                                                            Baadhi ya wananchi wa kata ya Masengwa waliohudhuria uzinduzi wa Kampeni hiyo 

                                                                            wakifuatilia kwa makini shughuli zinazoendelea uwanjani hapo

                                                                                          Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akitoa maneno ya 

                                                                                          ukaribisho kwa wageni waliohudhuria shughuli hiyo ya uzinduzi katika Wilaya ya Shinyanga

                                                                              Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga akitoa neno katika uzinduzi huo wa Kampeni ya kujiunga na CHF

                                                                           Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack pamoja na Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga 

                                                                           wakijumuika kucheza ngoma ya Kisukuma inayoongozwa na jeshi la Sungusungu la kijiji cha Ilobashi



                                                                  Mnufaika wa mfuko wa CHF tangu ilipoanzishwa na Serikali mwaka 2001, Bw. William Gwisu mkazi wa 

                                                                  kata ya Masengwa, akitoa ushuhuda wake jinsi mfuko ulivyomnufaisha na kuwamasisha wengine kujiunga

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa