• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWATAKA VIJANA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIELIMISHA ZAIDI

Posted on: July 20th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewataka vijan kuitumia mitandao ya kijamii kujielisha zaidi ili kupata maarifa yatakayo wawezesha kufanya kazi kwa ubunifu zaidi, kujitangaza na kutafuta masoko nje ya eneo lao la kazi.

Mhe. Mndeme ameyasema hayo leo tarehe 20 Julai, 2023 alipotembelea na kuzungumza na Kikundi cha Watengeneza Masofa kilichopo Kalola katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambapo pamoja na maelekezo mengine aliwasifia vijana hao kwa kazi nzuri wanazozifanya huku akiwata kuonesha shukurani zao kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya kazi zaidi baada ya kuwa wamenufaika na mkopo usiokuwa na riba wa Milioni 30.

"Kwanza niwapongeze sana kwa kazi nzuri za ubunifu mnazozifanya haoa katika karakana yenu, lakini niwatake sasa kutumia mitandao ya kijamii kujiongezea maatifa kwa kusoma, kujitangaza ninyi na bidhaa zenu na kutafuta masoko ili muweze kuuza ndani na nje ya Mkoa wa Shinyanga pamoja na nje ya nchi yetu kwakuwa kazi zenu ni nzuri sana," alisema Mhe. Mndeme.

Kando na hayo, pia Mhe. Mndeme akiwata vijana hao kutokubali kudanganywa na baadhi ya watu wanaoeneza maneno yasiyokuwa na ukweli kwamba nchi itauzwa au bandari inauzwa jambo ambalo siyo kweli kabisa, Serikali ipo makini sana na kilichofanika katika suala la Bandari ni mkataba wa makubaliano ya kuboresha utoaji wa huduma.

Kwa upade wake Ndg. Luhanya Anatory Sita ambaye ni Mwenyekiti wa Kikundi kwa niaba ya wenzie alimshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwakopesha Milioni 30 bila riba jambo ambalo limeborsha sana kazi zao. Kisha akamshukuru pia Mhe. Mndeme kwa kuwatembelea katika katakana yao huku wakisema kuwa kitendo hicho kinawapa moyo na imani kubwa sana kwamba Serikali ipo pamoja nao na ndio maana iliwakopesha fedha zisizo na riba ili kuboresha kaai zao.

Awali Mhe. Mndeme akiwa ameongozana na mwenyeji wake Mhe. Mboni Mhita alitembelea, kukagua na kushiriki kazi mbalimbali za kijamii ambapo alipalili eneo la kupandia miti 500 katika Zahanati ya Kijiji cha Masabi, kuteremsha tofali katika Kituo cha Afya Segese kitakachokuwa kinahudumia vijiji zaidi ya vitano na kukutana na wanafunzi ambapo aliwakumbusha wajibu wao wa kusoma kwa bidii kwani Serikali imekwisha walipia gharama zao zote.

Ziara hii ni hitimisho ya mfululizo wa siku 4 ambapo Mhe. Mndeme ambaye aliongozana na Kamati a Usalama ya Mkoa na ameweza kuzitembelea Halmashauri 6 zilizopo ndani ya Mkoa wa Shinyanga na kukagua miradi 42 itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru 2023 ambapo kwa ujumla wake ameridhishwa na maandalizi yote.

Mhe. Mndeme akimsikiliza mwenyekiti wa Kikundi cha Vijana Watengeneza Masofa Ndg. Luhanya Anatory Sita (wa tatu kutoka kulia) akielezea jambo kuhusu kikundi chao

Mhe. Mndeme akionekana kwenye picha wakati akishiriki shughuli mbalimbali za kijamii akiwa na Mkurugenzi wa Msalala Ndg. Khamis Katimba na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita









Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa