• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AWATAKA WAJUMBE WA BODI YA MAJI BONDE LA KATI KUFANYA UCHAGUZI KWA UAMINIFU NA UANGALIFU

Posted on: August 7th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka wajumbe wa Bodi ya Maji Bonde la Kati kufanya uchaguzi wa viongozi wao kwa umakini, uangalifu na uaminifu zaidi huku akisisitiza ushiriki wa wadau uwe madhubuti kwa kila mdau na kuhakikisha habaki nyuma katika kila zoezi litakalofanyika katika kikao hiki.

Mhe. Macha ameyasema haya leo tarehe 7 Agosti, 2024 alipokuwa akifungua kikao hiki cha wajumbe wa Bodi ambapo pamoja na mambo mengine pia amewataka wajumbe kubainisha na kujadili changamoto mbalimbali zilizopo katika kidakio cha maji Sibiti sanjari na kushirikiana kuhusu shughuli za usimamizi wa rasilimali za maji.

"Niwaagize wajumbe wa Bodi ya Maji ya Bonde la Kati kuhakikisha mnafanya uchaguzi wa viongozi wenu kwa umakini, uaminifu na uangalifu mkubwa ili lengo la Serikali na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi la kuhakikisha wananchi wanasogezewa huduma ya maji inafikiwa walau kwa asilimia 95 mijini na 85 vijijini ifikapo mwaka 2025 kama ilivuoahidiwa," amesema RC Macha.

Aidha RC Macha amesema kuwa, falsafa ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha anamtua ndoo mama kichwani inakwenda vizuri sana ambapo mpaka sasa Mkoa wa Shinyanga umepewa fedha zaidi ya Bil. 77 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji, yote inalenga utekelezaji wa maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Awali ndg. Julius Kagoma ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Bodi ya Maji Bonde la Kati alimueleza mgeni rasmi pamoja na wajumbe kuwa pamoja na mambo mengine wamekutana katika kikao cha Uundaji wa Kamati ya Kidaka Maji cha Sibiti (Sibiti Catchment Committee) ili kufanya uchaguzi wa viongozi pamoja na kuandaa mpango kazi utakaotumika kuongoza utendaji kazi wa Bodi itakayoundwa.

Kwa ujumla Bodi ya Maji Bonde la Kati iliyoundwa chini ya kifungu cha 22 cha Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na.11 ya mwaka 2009 na marekebisho yake Na. 8 ya mwaka 2022 inajukumu kuu la kusimamia rasilimali za maji ikiwemo utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa